channel logo dark
jiya, slim billboard,
channel logo dark

Jiya

160DramaPG13

Sababu tatu za kutoingia ndani ya mahusiano ya kimapenzi na bosi wako – Jiya

Habari
26 Septemba 2024
Dr Zaramo aanza kumuwazea mate wafanya kazi wake, Neshapai na Maua.
Article

Ndani ya kipindi cha Maisha Magic Bongo, cha "Jiya," tunaona mfano wa jinsi uhusiano wa kimapenzi na bosi unavyoweza kuleta matatizo. Dr. Zaramo, daktari mwenye ushawishi, ameanza kuashiria kwamba angetaka kumchumbia muuguzi anayefanya naye kazi, Neshipai. Mbali na Neshipai, Dr. Zaramo pia ameanza kumpa zawadi msichana wake wa kazi, Maua, na kumtongoza. Mahusiano kazini sio kitu kinachopendezesha na pia mahusiano na bosi wako yanaweza kuleta matatizo kwako. Soma sababu tatu mbaya zinanzo weza kutokea ukiwa na mahusiano na bosi wako:

  1. Kuchumbiana na bosi kunaweza kusababisha mgongano wa maslahi.

Uhusiano huu unaweza kuathiri utendaji wa kazi na kuleta ubaguzi. Wafanyakazi wengine wanaweza kuona kuwa Neshipai anapendelewa kwa sababu ya uhusiano wake na Dr. Zaramo, jambo ambalo linaweza kuharibu mazingira ya kazi na morali ya wafanyakazi.

  1.  Hatari ya kunyanyaswa kimapenzi.

Neshipai na Maua wanajikuta katika hali ngumu ambapo wanahisi kulazimishwa kukubali mapenzi ya Dr. Zaramo ili kulinda kazi zao. Hii ni aina ya unyanyasaji wa kimapenzi ambayo inaweza kuwa na athari mbaya kwa afya yao ya kiakili na kihemko.

  1.  Mahusiano haya yanaweza kusababisha masuala ya kisheria.

 Ikiwa Neshipai au Maua watashindwa kupata haki sawa kazini kutokana na mapenzi ya Dr. Zaramo, wanaweza kuchukua hatua za kisheria dhidi yake na kampuni. Hii inaweza kusababisha hasara kubwa kwa Dr. Zaramo na sifa mbaya kwa taasisi nzima.

Mahusino na bosi wako - Jiya

Je wewe unaweza kuingia ndani ya mahusiano ya kimapenzi na bosi wako?

Click here to make your selection
Hapana
Ndiyo

Hali ya Dr. Zaramo, Neshipai, na Maua inatufundisha umuhimu wa kuweka mipaka kati ya maisha ya kikazi na ya kibinafsi ili kulinda heshima na haki za kila mmoja. Endele kufuatilia #MMBJiya kila Jumatatu hadi Jumatano saa 1:30 usiku ndani ya DStv chaneli 160.